Posts

37. WAITWA, MWOVU NA BWANA

WAITWA, MWOVU NA BWANA 1.   W aitwa, mwovu, na Bwana Umwendee hima sana, Usafiwe dhambi zako, Humwoni ni mwema kwako? Chorus: Unaitwa! Itika tu! Umwendee Bwana Yesu! Sifiche makosa yako, Uungame dhambi zako! Kristo tu umuamini, Ndiyo njia ua Mbinguni.   2.    Alilipa damu yake Alikufa yeye Bwana, Mimi nawe tuwe wema.   3.    Ukifanywa kuwa mwema Utaingia rahani Na wapenzi wa zamani.   4.    Ni mwanga tu, nchi ile, Kwamba wataka ufike Sharti huku uosheke.

38. TWENDE KWA YESU

TWENDE KWA YESU 1.    Twende kwa Yesu mimi nawe, Njia atwonya tuijue Imo Chuoni; na Mwenyewe, Hapa asema, Njoo!   Chorus: Na furaha tutaiona, Mioyo ikitakata sana, Kwako, Mwokozi, kuonana, Na milele kukaa.   2.    “Wana na waje”, atwambia, Furahini mkisikia, Ndiye mfalme wetu pia, Na tumtii, Njoo.   3.    Wangojeani? Leo yupo; Sikiza sana asemapo; Huruma zake zikiwapo, Ewe kijana, Njoo.

39. MWENYE DHAMBI HUNA RAHA

MWENYE DHAMBI HUNA RAHA 1.    Mwenye dhambi huna raha, Sikiza nakusihi, Utapata msamaha Kwake Yesu Mwokozi! Njoo hima, njoo hima, Naye atafurahi.   2.    Yesu anakwita sana Naye yuko Mbinguni; Hofu ya kifo hapana Kwake ukiamini. Njoo hima, njoo hima, Utapata amani.   3.    Hatakwita siku zote; Ni ya sasa nafasi. Lete na uchafu wote, Kukawa haipasi. Njoo hima, njoo hima, Ni wokovu halisi.   4.    Uzima uko kwa Bwana Twae uzima hasa Bure unapatikana, Wokovu twae sasa! Njoo hima, njoo hima, Twae utakatifu.

40. NASIKIA KUITWA

NASIKIA KUITWA 1.    Nasikia kuitwa Na sauti yako Nikasafiwe kwa damu Ya kwangikwa kwako. Chorus: Nimesogea Mtini pako, Unisafi kwa damu ya kwangikwa kwako.   2.    Ni mnyonge kweli, Umenipa nguvu, Ulivyonisafi taka, Ni utimilivu.   3.    Yesu hunijuvya; Mapenzi imani, Tumai, amani, radhi, Hapa na Mbinguni.   4.    Huipa imara, Kazi yake, ndani: Huongezeka neema, Ashindwe Shetani.   5.    Huishuhudia, Mioyo ya imani Ya kuzipata ahadi, Wakimuamini.   6.    Napata wokovu, Wema na neema; Kwako Bwana nina nguvu Na haki daima.

41. YESU ALINIITA

YESU ALINIITA 1.    Yesu aliniita, “njoo, Raha iko kwangu, Kichwa chako ukilaze Kifuani mwangu.” Nilikwenda kwake mara, Sana nilichoka, Nikapata kwake raha, Na furaha tena.   2.    Yesu aliniita, “njoo, Kwangu kuna maji, Maji ya uzima, bure, Unywe uwe hai, ” Nilikwenda kwake mara Na maji nikanywa; Naishi kwake, na kiu Kamwe sina tena.   3.    Yesu aliniita, “njoo, Dunia ni giza, Ukinitazama nuru Takung’arizia.” Nilikwenda kwake mara Yeye jua langu, Ni kila wakati mwanga Safarini mwangu.

42. KIVULINI MWA YESU

KIVULINI MWA YESU 1.    Kivulini mwa Yesu kuna Kituo: Kituo mbali na hamu, kituo kilicho tamu.   Chorus: Kivulini mwa Yesu kuna kituo; Kivulini mwa Yesu kuna kituo; Raha tu, mle; amani tupu. Furaha tele; kivulini mwa Yesu Raha tu, mle; amani tupu, Furaha tele; kivulini mwa Yesu.   2.    Kivulini mwa Yesu nina amani Iliyopita fahamu, tena itakayodumu.   3.    Kivulini mwa Yesu nina furaha; Furaha yenye fahari, ya kueneza habari.

43. YESU AKWITA

YESU AKWITA 1.    Yesu akwita, chanena Chuo; Uje leo, uje leo; Kwani kusita? Akwita, Njoo; Unatanga upeo. Chorus: Hwita leo, hwita leo. Yesu akwita kwa pole akwita leo.   2.    Waliochoka, wapumzike, Hwita leo, hwita leo: Wenye mizigo, wakamtweke, Wapate mapumuo.   3.    Anakungoja, uliye yote, Uje leo, uje leo; Uliyekosa usijifiche: Woshwe, uvikwe nguo.   4.    Yesu asihi wakawiao, Waje leo, waje leo. Watafurahi waaminio; Usije kwani? Njoo.